Journal Category
Journal Archive
- April 2007 (1)
- March 2007 (1)
- October 2006 (3)
- September 2006 (1)
Journal
Thursday,Oct 19 2006, 02:07:40 PM Machifu
Sijuwi tuanzie wapi ndugu zangu ili mpate kutuelewa
Walikuwa ni machifu wetu wa Tanganyika, heshima.
Wakiongozwa na simba wa nyika, heshima.
chifu Kinjeketile Ngwale mwana wa rufiji, yeye yeye
muanzishaji wa vita vya maji maji , uuhh,
na aliyetaka risasi kuzigeuza maji, heey
ni pale, waliponyanyaswa na kutweswa tena zion
jamani, waliingiwa na ile roho ya lion
e e eee wakatangaza vita na mababilon
wasukuma kwenye pamba walianzisha mgogoro , oohooo
wakiongozwa na chifu Makongoro
wachagga wao waliibuka kwenye mikahawa na kuwafanyia kweli , we
walikuwa na machifu Sina na mangi Meli
wangoni waliwapiga na wakaiteka peramiho bila huruma, yeah
pamoja na machifu Songea na Chabruma
kwa wamachinga mababilon waliingia na kutaka kujichanganya, waliumia
wakakumbana na chifu wao Makunganya,
ni pale, waliponyanyaswa na kutweswa tena zion
jamani, waliingiwa na ile roho ya lion
e e eee wakatangaza vita na mababilon
waliingia musoma na kukuta watu wamekwisha waona na kuwasoma
na kwa wakerewe wakakutana na chifu Lukonge, loh
wataalamu wanasema mganga akipata dawa wanga wanapagawa
wakaamua kuikimbia Mara maana ilikuwa imaraaa
kwa wahehe hata wale waliovaa kitasha waliuliwa,
waliongozwa pomaja na chifu Mkwawa, sawsawa
wazaramo wao walishajua kuwa mababilon wana hila,
mapema waliwatandika wakiwa pamoja na chifu wao Kibasila , tunakwambia
ni pale, waliponyanyaswa na kutweswa tena zion
jamani, waliingiwa na ile roho ya lion
e e eee wakatangaza vita na mababilon
wafipa nao hawakukaa peke yao bali waliwasaida wenzao,
na chifu Kimalaunga akiwa pamoja nao.
wayao nao kitambo walishakaa chemba pamoja na chifu wao Machemba
wanyamwezi pamoja na chifu Isike ,
wapogoro na wandengereko nao pia walikuwepo, uwoo
mababilon cha moto walikiona toka kwa machifu wetu
na huo ndio ulikuwa mwanzo wa heshima kwetu uuuooo Jah
ni pale, waliponyanyaswa na kutweswa tena zion
jamani, waliingiwa na ile roho ya lion
e e eee wakatangaza vita na mababilon

